CHAMA CHA WAONGOZAJI (DIRECTOR) MKOANI DAR ES SALAAM WAANDA SEMINA
habari, mpya, slide 10:45 PM
Sehemu ya waongozaji (director) waliyofanikiwa kufika katika semina wakifuatilia kwa ukaribu zaidi mafunzo toka kwa wakufunzi toka pale chuo kikuu cha Dar es salaam, semina hii imetayarishwa na kuratibiwa na shirikisho la filamu Tanzania TAFF kupitia chama cha waongozaji chini ya mwenye kiti wake ndugu Paul Mtendwa na usaidizi wamakamu wake bwana John Rista,
Semina hii ya siku tatu imetayarishwa na kufanyikia pale Balaza la sanaa taifa (BASATA) ndani ya ukumbi wa ndani wa miokutano mahususi kwa waongozaji kuweza kutambua mambo ya msingi mwongozaji anayopaswa kuyafahamu anapokuwa kwenye mchakato wa utayarishaji picha jongefu(filamu) kama kusoma na kundua tabia za nje na za ndani za wachezaji picha ile ili kumrahisishia shughuli yote kwa ujumla wake, kufahamu namna ya kuunganisha nakuhusisha matukio moja baada ya njingine kulingana na muswada wa hadithi husika katika ungozaji wake,kuanda vizuri hadithi yake ili afahamu idadi ya matukio yatakayotengenzwa.
Hizi picha hapo chini ni baadhi ya picha za waongozajipicha waliyofika hapo balaza la sanaa taifa kuhudhulia na kupata mafunzo hayo yaliyoandaliwa... Ndugu, Simon Mwakifamba (Rais wa shirikisho la filamu tanzania Taff) akifafanua jambo kwa waongozaji waliyohuzulia semina hiyo....