WINO WA MWANDISHI

MZEE MAJUTO: WASANII WOTE HUSAFIRIA NYOTA YANGU

Iko wazi kabisa si kipaji tu cha mzee majuto ndicho wasanii wenzeka katika tasnia ya maigizo hapa nchini wanakihitaji katika filamu zao...

01 Jul 2014 / 0 Comments / Soma zaidi
WINO WA MWANDISHI

MJUE VILIVYO HASHIM KAMBI

Kama unafuatilia sanaa ya filamu nchini Tanzania, sina wasiwasi kwamba sura unayoiona hapo juu unaitambua. Unachoweza kuwa hukijui ni j...

09 Aug 2012 / 0 Comments / Soma zaidi

AFRICA MAGIC SWAHILI WAFANYE MABADILIKO



Kuanzishwa kwa Channel ya AMS (Africa Magic Swahili) kulikuwa sehemu ya mabadiliko makubwa katika tasnia ya filamu hapa nchini. Hii ina maana filamu zetu hazitaishia kuonyeshwa na ITV, Channel 10, Channel 5, TBC 1, C2C, Clouds TV, Mlimani TV, na kahdalika.
Mabadiliko hayo sio kusmimuliwa kupitia redio zetu pekee, bali hatua kubwa kwa waigizaji wenyewe na kazi zao. Pia manufaa kwa Africa Magic Swahili kwa kufanya biashara nzuri na yenye tija kwa nchi za afrika mashariki.
Tunajua kuwa fasihi ni kazi ya sanaa inayotumia lugha kufikisha ujumbe wake. Vilevile Africa Magic Swahili ni sehemu ya jamii kwahiyo kujitokeza hadharani kulikuwa na maana wamejiandaa kukosolewa, kusifiwa na kukubalia kuwa wabunifu zaidi.
Kuna mambo mazuri sana katika Africa Magic, pia kuna mambo mengine sio mazuri kabisa kwakuwa imekuwa kero zaidi. Bahati nzuri suala hilo halipo kwa wapenzi wa filamu nchini pekee, bali hata kwa waigizaji.
Waigizaji wanapofika mahali wanakosoa mwenendo wa Africa Magic Swahili, ambayo mwanzoni walishangilia ujio wake, basi ujue kuna tatizo katika tasnia ya filamu na shime wahusika wanatakiwa kufanyia kazi.
Mimi nimekuwa mdau mkubwa katika Channel hiyo, ninaweza kusema kifupi tu, siridhishwi na kazi zinazoonyeshwa. Sio rahisi kuwananga Africa Magic kuwa hawajali au hawaelewi maana ya kuwa makini.
Lakini lazima wabadilike zaidi na wafanye jitihada kuwashawishi waigizaji wakubwa kuwasilisha kazi zao kituonni hapo. Kwanini ninasema hivi?
Hivi karibuni mwigizaji hodari wa filamu nchini Jacob Steven(JB) amelalamikia kituo cha Africa Magic kutoa malipo kidogo kwa kazi zinazowasilishwa.
JB anadai kuwa malipo madogo yanayotolewa na kampuni ya Maultichoice kutokana na kazi zao zinazoonyeshwa Channel ya Africa Magic Swahili inasababisha baadhi yao waache kupeleka kazi zao katika channel hiyo.
JB alikaririwa akisema, baadhi ya filamu zinazoonyeshwa Africa Magic Swahili hazina ubora wa kutosha. JB anaongeza kuwa matokeo yake watazamaji wa hapa nchini na nje wanadhani filamu za Tanzania ni nyepesi au rahisi mno kadiri wanavyoziona, kumbe kuna filamu bora zaidi hazipelekwi Africa Magic Swahili kwakuwa malipo ni madogo sana.
JB alikaririwa akisema, “kwanza kabisa leno la kuanzishwa kwa stesheni ile ilikuwa ni kukikuza kiswahili matokeo yake inaonekana kwenye nchi za afrika mashariki ambazo baadhi wanakijua Kiswahili hivyo ili iwe na maana iende mbali ivuke ndio lengo la kukitangaza Kiswahili litatimia”. Aidha, alikaririwa pia akisema; “kwa malipo wanayolipa si rahisi kupata kitu ambacho wamekusudia ili waweze kuzitangaza filamu za Tanzania ni bora wakaongeza mapato lakini kwa ilivyo sasa ni sawa na kutoa bure ingawa ni mkataba na makubaliano maalumu lakini bado ni kidogo sana”.
Bahati nzuri ni kwamba Ofisa Uhusiano wa Multchoice, Barbara Kambogi ameeleza kuwa suala hilo ni miongoni mwa changamoto zinazofanyiwa kazi na akaongeza kusema masafa ya stesheni hiyo yanafanyiwa marekebisho ili yaweze kufika nchi zingine.
Kwanza namuunga mkono JB kwa msimamo mkali, na pili tumuunge mkono Bi Kambogi kwa uungwana wake kukiri na kusema mabadiliko yatakuja tu katika masuala hayo. Jambo muhimu hapa ni Multchoice kuelewa kuwa idadi ya watumiaji wa huduma ya kulipia ya DSTV imekuwa kubwa, sababu filamu za Tanzania zinapendwa na watanzania wenyewe.
Kwahiyo hatua ya watanzania kupenda kumiliki huduma za DSTV maana yake inatakiwa Africa Magic Swahili iende kwa wakati katika ushindani wa soko la filamu. Changamoto nyingine ni kulipia huduma za DSTV kwa kutumia dola badala ya shilingi. Hii ni changamoto kubwa kuliko zote,
Maana suala la mwigziaji wa filamu JB unaweza kumwita na kutengeneza mkataba mnono naye akakubali kisha kuchukua kitita chake. Lakini suala la kulipia huduma hiyo kwa dola badala ya shilingi ni tatizo jingine kubwa mno.
Katika suala filamu lazima tukiri bado hatujaona filamu bora tunzoona mitaani zikionyeshwa Africa Magic Swahili. Baada ya kujiuliza sana nadhani sasa JB anatupatia majibu na kuifahamisha jamii kuwa kuna unyonyaji na lazima ufanyiwe kazi.
Pengine Multchoce inashindw akugundua jambo moja muhimu sana. Multchoice inaweza kuwachukua waigizaji fulani na kuingia nao mkataba ili filamu zao zionyeshwe katika stesheni yao, yaani kama unaona JB ana soko kubwa katika filamu basi yeye anatafutwa na kupewa mkataba mnono ili filamu zake zinapotengenezwa moja kwa moja zinaingia kwenye rada za Multchoice badala ya kungojea watu wanazungumziaje au idadi ya w apenzi wa filamu yake wanavyojisikia.
Au Multchoice inaweza kujiingiza katika soko la filamu kwa kumiliki waigizaji wake kwa mkataba maalumu. Waigizaji hao watakuwa wakifanyia kazi katika kampuni yao, wachukua mfano wa Sony, 20th Century Fox, Paramount Pictures, SpyGlass, au Universal Channel.
Hiyo ni mifano midogo tu, kwani itasaidia kuepuka malalamiko kama hayo. Pia Multchoice inapokuwa na waigizaji wake maana yake inakuwa na uwanja mwingine wa kuingia mikataba na waigizaji wan je ya kampuni yao.
Ni rahisi, ikiwa utafiti wa kibiashara na masoko utafanywa. Vinginevyo Africa Magic Swahili inapaswa kuwasikiliza waigizaji na ipange kiwango bora cha malipo kwa waigizaji bora na filamu bora, sio kila filamu ionyeshwe Africa Magic Swahili.

Na Markus Mpangala
[Mdau Wetu]
Asante!

Posted by bongofilmdatabase on 11:47 AM. Filed under , , , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0

0 comments for AFRICA MAGIC SWAHILI WAFANYE MABADILIKO

Post a Comment

LETS HOOK UP

.

.
.

SIRI YA MTUNGI PHOTO CAPTION


Recently Commented

ALBUM YA BONGOFILM

HABARI MPYA INAVYOSEMEKANA WADAU
KUTA ZA FACEBOOK

WASAMBAZAJI HEWA

Wasambazaji hewa ni yupi kati huyu? A.Steps B. Proinkiini cha taarifa za filamu bongo...

19 Jun 2016 / 0 Comments / Soma zaidi

FILAMU ZA BONGO NI MAIGIZO YA MAISHA YA WAPI?

kiini cha taarifa za filamu bongo...

01 Jul 2014 / 0 Comments / Soma zaidi

YASEMEKANA HUU NDO MWANZO NA ILIPOANZIA VAMPIRE DIARIES

The Vampire diaries tamthilia yakusisimua sana iliyojizolea mashabiki kibao hapo nchini na mataifa mengi dunia inasadikika kuwa mwanzo w...

28 Nov 2013 / 0 Comments / Soma zaidi

BADO SIKU CHACHE TU! karibuni wadau wote

Asanteni sana wadau wetu kwa kutuunga mkono siku zote hizi tangu tuanzishe kurasa wetu huu wa Bongo Film DataBase..Tumesikiza na tuanyafa...

25 Nov 2013 / 0 Comments / Soma zaidi
FILAMU MPYA

BODY GUARD NI MIONGONI MWA FILAMU KALI TOKA ASIA MWAKA HUU.

  Body Guard ni moja ya filamu zinazopigiwa kura nyingi sana kwa mwaka huu na wafuatiliaji filamu hizi za kihindi....

08 Apr 2013 / 0 Comments / Soma zaidi

GELLY WA RHYMES ATUPA KARATA NYINGINE KWENYE LIMBWATA

GELLY WA RHYMES Mwanamuziki/Mwigizaji LIMBWATA NI HADITHI YA BINTI MMOJA ALIYETOKA KIJIJINI KUJA MJINI KUTAFUTA AJILA  NA...

17 Nov 2012 / 0 Comments / Soma zaidi

SIMULIZI ZILIZOBAMBA KWENYE KURASA ZA KIJAMII

TAKE ONE -HBABA NA FLORA INTERVIEW

SIMULIZI

SIMULIZI SEHEMU YA PILI

DADA POA..SEHEMU YA KWANZA,PILI NA YA TATU...SIKILIZA SIMULIZI HII YA KUSISIMUA, INAYOHUSU MAISHA YA MWANADADA ....MANKA..Bofya kiunga h...

26 Jul 2013 / 0 Comments / Soma zaidi

SIMULIZI NA ADELA KAVISHE

DADA POA..SEHEMU YA KWANZA,PILI NA YA TATU...SIKILIZA SIMULIZI HII YA KUSISIMUA, INAYOHUSU MAISHA YA MWANADADA ....MANKA.. Bofya kiu...

26 Jul 2013 / 0 Comments / Soma zaidi
BOLLYWOOD

BODY GUARD NI MIONGONI MWA FILAMU KALI TOKA ASIA MWAKA HUU.

  Body Guard ni moja ya filamu zinazopigiwa kura nyingi sana kwa mwaka huu na wafuatiliaji filamu hizi za kihindi....

08 Apr 2013 / 0 Comments / Soma zaidi

GELLY WA RHYMES ATUPA KARATA NYINGINE KWENYE LIMBWATA

GELLY WA RHYMES Mwanamuziki/Mwigizaji LIMBWATA NI HADITHI YA BINTI MMOJA ALIYETOKA KIJIJINI KUJA MJINI KUTAFUTA AJILA  NA...

17 Nov 2012 / 0 Comments / Soma zaidi
BONGO MOVIE

MONALISA, KING MAJUTO NA BARAFU NDANI YA DALADALA MOJA

Mwigizaji Yvonne Cherryl au mwite Monalisa kupitia ukurasa wake facebook amepost picha kadhaa zikimwonesha yeye na waigizaji wenzake...

26 Jul 2013 / 0 Comments / Soma zaidi

DUME JEURI NI MKOMBOZI NA IMEIBUA HISIA CHANYA KWA WALIOPUUZWA

Uwezo wa msanii huzihilika pale apewapo nafasi bila kutiliwa shaka nae hujisikia ni msanii muhimu kwenye kuikamilisha filamu mpaka i...

25 Jul 2013 / 0 Comments / Soma zaidi
SERIES KALI

ZIJUE SERIES ZILIZOTAMBA NA ZINAZOBAMBA KWA SASA UKIANZIA NA YA ARROW ( Eps 1 )

Katika nyumba tano hapa mjini kwa sasa iishiyo vijana wapendao filamu zitokazo hollywood basi nyumba mbili kama sio tatu katika ya hizo ...

08 Apr 2013 / 0 Comments / Soma zaidi

UANDISHI WA FILAMU NA MAIGIZO

UANDISHI WA FILAMU NA MAIGIZO JIFUNZE NAMNA YA KUANDIKA NA KUANDAA SCRIPTS MUUNDO WA HADITH SEHEMU YA PILI  2. MUUNDO WA ENE...

01 Feb 2012 / 2 Comments / Soma zaidi

2009 Bongofilmdatabase. All Rights Reserved. - Designed by Oscar kwa ushirikiano wa SimplexDesign