WEMA ;MAISHA YANGU NI BIASHARA NA SEHEMU YA KUONGEZEA UMAARUFU KWAO


 Kwa takwimu isiyopingika kwa wasomaji magazeti na watumiaji mitandao ya kijamii ya kuwa Bi dada Wema atakuwa anaongoza sasa kwa kuandikwa na kutajwa sana kwenye vyombo vya habari taklibani vyote kuliko wasanii wote hapa nchini tangu huu mwaka uanze mpaka sasa. ilifikia wakati gazeti linalochapisha taarifa na habari za mwana dada huyu lilikuwa halifiki majira ya mchana linakuwa limekwisha kwenye vibanda na meza za kuuzia magazeti magazeti hayo ya kinunuliwa kama njugu ndani ya muda mfupi sana. 

Hali hii ikapelekea abatizwe jina la Wema a Queen of Scandle hapa Bongo kitu ambacho wamiliki wa vyombo vya habari hivi walimpamba kwa jina hilo kwa lengo la wao kuendelea kusukuma kama sio kubakia na mstari ule ule wa mauzo ya bidhaa zao kuanzia magazeti , kutizamwa na kusiklizwa kwa vituo vyao vya kurushia matangazo..  

Kiukweli hali hiyo ilimpelekea mwana dada huyu kupata ujasiri wa kipekee sana wa yeye kujiamini huenda sasa anaweza kuanda kazi zake na zikauza sana kama asivyo kauka vinywani mwa watu?  hivyo kuamua kuanda filamu yake ambayo kwa asiliamia tisini kama siyo themanini na tano itazungumzia maisha yake ya hapo nyuma na sasa kuanzia kwenye umiss na maisha yake ya mapenzi uhususani penzi lake hili la mwisho ambalo nalo lilichangia sana yeye na x-boyfriend wake kuandikwa na kutajwa sana mitaani kila kulipokucha na  zaidi hasa pale walipokuwa kwenye mtafaluko katika mahusiano yao.


Sehemu moja wapo katika filamu hiyo pana sehemu ambayo ataonekana boy freind wake wazamani  akivisha pete wema kwenye moja ya kumbi za starehe hapo mjini dar es salaam uliyopo huko masaki katika taswira nyingi ila lengo ni kuupata wakati ule ule kama ilivyokuwa siku ile xboy alivyofanya.  kuvishwa pete ya uchumba na msanii wa bendi ya Machozi, anayekwenda kwa jina la Mwinyi ndiyo tukio lillilobeba vichwa vya habari vya magazeti tena na kuongeza mauzo tena kama ilivyokuwa pale awali.

Tukio hilo ambalo lilivuta hisia za wapenzi wa masuala ya udaku na burudani nchini, lilijiri katika ukumbi huo. ukweli ambao umewekwa wazi ni kuwa, mwanadada huyo alihusika katika tukio hilo kama sehemu ya maandalizi ya filamu yake mpya itakayokwenda kwa jina la Super Star akiwa amesimama kama muhusika mkuu na na mtayarishaji filamu hiyo.

Movie hiyo inatarajiwa kuelezea maisha halisi ya msanii huyo ambaye pia aliwika katika medani za ulimbwende, na Mwinyi atashiriki katika filamu hiyo akiigiza nafasi ya mwanamuziki Diamond, ambaye alikuwa mpenzi wa Wema na ambaye alimvisha pete ya uchumba lakini wakamwagana baadae kutokana na mikasa baina yao kuzidi kushamiri.

Kibwagizo: Hata hivyo, Wema anajulikana kuwa hajatulia, unadhani itashangaza kesho kusikia kuwa tukio hilo mbali ya kuwa sehemu ya filamu, lilikuwa pia tukio rasmi la kuwaunganisha wawili hao?

Posted by bongofilmdatabase on 10:26 AM. Filed under , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0

0 comments for WEMA ;MAISHA YANGU NI BIASHARA NA SEHEMU YA KUONGEZEA UMAARUFU KWAO

Post a Comment

LETS HOOK UP

.

.
.
slide

SIRI YA MTUNGI PHOTO CAPTION


Recently Commented

ALBUM YA BONGOFILM

SIMULIZI ZILIZOBAMBA KWENYE KURASA ZA KIJAMII

TAKE ONE -HBABA NA FLORA INTERVIEW

2009 Bongofilmdatabase. All Rights Reserved. - Designed by Oscar kwa ushirikiano wa SimplexDesign