JACKLINE WOLPER AKANUSHA UVUMI WA MAGAZETI YA UDAKU

Hivi karibuni BONGO FILM DATA BASE ilipendezwa sana na mtindo wa nywele anaoutumia dada Jackline na kusema ''hivi ndivyo msanii anapaswa kuwa mwonekano tofauti tofauti yaani kubadilika badilika kama kinyonga''. loh! basi kwa upande wa pili wa shilingi, jamii ilijawa hofu, kama sio kupigwa na butwaa kubwa juu ya habari hii sana kwa wale walio pata kusikia na kuona kupitia baadhi ya vyombo vya habari mahiri hapa nchini vitupatiavyo taarifa kede kede za nyota wetu kwa jina mahili ya vyombo hivyo huitwa ''UDAKU''

Kwenye ukurasa wa mbele kabisa wa vyombo vya udaku uliliwekwa uwazi wa tukio hili kwa mfumo wa picha na kuelezea kwa kina zaidi picha hizo ndani ni kwa namna gani wasani wetu wa kibongo wanonekana katika jamii yetu ya sasa kwa kudandia mambo wasio ya jua madhara wa faida zake kutoka mataifa ya ughaibuni ya sio kuwa na maadili mbele za mboni zetu hasa hizi za macho ya kiafrika,mambo mengi wanayofanya wasani wa kitanzania na afrika kwa ujumla daima huwa ni ya kugeza toka balani uraya kama sio marekani tukianzia mavazi,mitindo ya nywele,namna wanvyo igiza,imba,na hata uchezaji wa miziki na mengine kadhalika yanayofanania na hayo.

kwa ubinafsi wetu tunasema kugeza kitu si mbaya kabisa tena mtu anapokuwa ana kiu ya kujua jambo daima hutawaliwa na nafsi moja tena iliyo kuu ya kwa nini yeye anaweza na mie nisindwe? na hatimaye anatahidi kugeza moja kwa moja na hata kumpita mwanzilishi wa hilo jambo.

Na pia kujifunza kitu kupo kwa mifumo mingi sana, tunapokuja kutizama upande wa sanaa yote kwa ujumla wake mfano kuigiza mwalimu huwaonesha namna mtu anatakiwa kuwa au kuigiza anapokuwa amekasilishwa na wanafunzi hurudia kitu hicho pia kwa kuona,kutafakari na hatimaye kutenda sasa walicho funzwa...

Na hata tukizingatia hao wenzetu wamekwisha piga hatua kubwa mbele kwenye nyanja karibia zote hivyo ufahamu wa baadhi ya mambo wanyo yafanya daima huwa na makusudi fulani katika maisha yao tukianzia suala la kibiasha na mwisho kujifurahisha nafsi,




Amber Rose ni msichana ambaye huenesha maisha yake kwa kutengemea vituko afanyavyo huko mitaani kwao ambavyo humwogezea thamani katika shughuli azifanyazo kwa upane wa UMODO hivyo kugeza kwetu nina imani si kwa kubomoa moja kwa moja kujenga na kulisongesha guludumu hili la sanaa mbele tu na si kingine jamani. kupitia mtandao wa kijamii mwadada Jackline akanusha manno yote yaliyoandikwa na kwenye kurasa za za UDAKU wiki iliyopiita ambazo zilisema maneno yafuatayo....

.........(NA NUKUU)........

''MUONEKANO mpya wa staa wa filamu za Kibongo, Jacqueline Wolper Masawe unaomfanya kufanana ‘kopiraiti’ na modo ‘chakaramu’ wa Kimarekani, Amber Rose kuanzia umbile, pozi tata na unyoaji wa nywele na kubaki kipara, umezua gumzo na sasa anang’ang’aniwa na msala wa picha za utupu.

Awali The Udaku Master, Ijumaa liling’atwa sikio na sosi wake kuwa Wolper amebandikwa jina la Amber Rose wa Bongo kufuatia ‘laifu staili’ yake kufanana na ile ya Amber orijino mwenye sifa kuu ya kupiga picha za utupu na kuziuza kwenye majarida na mitandao ya ‘mambele’.


SIYO KUNYOA TU
“Watu wanazungumzia kunyoa tu kwa sababu ndicho kinachoonekana kwa haraka. Ukweli ni kwamba ukimchunguza kwa ukaribu utagundua vitu anavyofanya vinafanana sana na Amber.

“Hata ukiingia mtandaoni, watu wakimuona Amber akiwa kwenye pozi za utupu mawazo yao yanakimbilia kwa Wolper kwa sababu wanafanana kwa sasa.

HOFU
“Hofu iliyotanda ni kwamba kama Wolper atakuwa anamuiga Amber kwa kila kitu, basi kuna uwezekano naye akaingia kwenye mkumbo huo wa kupiga picha za utupu ili kujiongezea kipato na matokeo yake atapoteza heshima mbele ya jamii kwani kupiga picha za utupu ni aibu kubwa''.


.............(MWISHO WA KUNUKUU)............

Da Jackline akanusha yote hayo na kueleza yaliyo ndani ya kichwa na moyo wake juu ya hili suala hapo juu kama ilivyo chapishwa kwenye kurasa za za UDAKU..Tarehe kumi na nne(14) mwezi huu asubuhi na mapema.

JACKLINE WOLPER; "SIJAMUIGA AMBER, JAPO SINA TOFAUTI NA AMBER ROSE KIMWONEKANO NA HAYO WANAYO YA SEMA KUHUSU PICHA ZA UTUPU NI YA KWAO TU KWENYE HIZO KUMPYTA ZAO MIE KAMA MSANII NTAENDELEA KUFANYA SHUGHULI ZANGU ZA SANAA NA BILA YA KUSAHAU KUYAZINGATIA MAADILI YA MTANZANIA "

Posted by Bongo Film Data Base on 4:44 AM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0

3 comments for JACKLINE WOLPER AKANUSHA UVUMI WA MAGAZETI YA UDAKU

  1. Thats a good post jamani

  2. nice site..

  3. bright colored web site experience
    http://www.refreshtalent.com/node/522920/
    http://www.museoconserva.es/node/3933
    http://www.refugiosoldenoche.com.ar/?q=node/312832/

Post a Comment

LETS HOOK UP

.

.
.
slide

SIRI YA MTUNGI PHOTO CAPTION


Recently Commented

ALBUM YA BONGOFILM

SIMULIZI ZILIZOBAMBA KWENYE KURASA ZA KIJAMII

TAKE ONE -HBABA NA FLORA INTERVIEW

2009 Bongofilmdatabase. All Rights Reserved. - Designed by Oscar kwa ushirikiano wa SimplexDesign