SERIKALI YATOA NEMBO YA KUZITAMBUA KAZI ZA WASANI SASA...


Nembo ya Bodi ya filamu
Nembo ya ukaguzi wa filamu, lazima kila filamu iwe na alama hii.
BODI ya ukaguzi wa filamu Tanzania kuanzia sasa itakuwa ikitokea alama ianyoonyesha kuwa filamu husika kuwa imekaguliwa na kupewa daraja husika, Wakiongea na FC mtendaji wa Bodi hiyo amesema kuwa alama hiyo ni muhimu sana kuonekana katika filamu yoyote inayoonyeshwa kwa jamii, na iwapo filamu itakosa alama hiyo basi ni filamu batili.
Nembo ya ukaguzi  wa filamu
Nembo ya ukaguzi wa filamu Tanzania.
“Nembo ambayo bodi inatoa ni kwa ajili ya utambuzi, inatakiwa ionekane katika filamu inapoaanza mwanzo, na mwisho wa filamu inapoisha, lakini pia alama inatakiwa kuonekana juu ya kava la filamu husika jambo litamtambulisha mnunuzi na mtu mwingine kuwa filamu hiyo imekaguliwa na kupewa daraja,”anasema mtendaji huyo.
Baada filamu kukaguliwa upewa daraja na kupewa kibali cha mwaka mmoja kwa ajili ya kuingia sokoni, wengi wanasema faida ya ukaguzi ni kupata filamu zenye maadili mema, pamoja na kutambua uwepo wa tasnia hii ya filamu Tanzania.
Wadau wa filamu
Picha ya Wadau wa filamu Bongo. wakiwa katika picha ya pamoja.
Gharama za ukaguzi ambayo imewekwa na Serikali ni Tshs. 1,000/= kwa dk. Lakini kwa filamu zinazotengenezwa na wageni hutozwa kwa fedha za kigeni, ni fursa nyingine kwa watayarishaji kuweza kupeleka filamu zenu zikaguliwe, kwani filamu hizo nyingi zimetengenezwa kwa kukiuka sheria ya utengenezaji filamu.
Kabla ya kutengeneza filamu ni lazima mtayarishaji apeleke muswada kwa ajili ya ukaguzi, baada ya ukaguzi wa muswada hatua inayofuatia ni uombaji wa kibali kwa ajili ya kurekodi filamu husika ambacho gharama yake ni TShs. 500,000/= na baadae tena filamu inarudishwa kwa ajili ya kukaguliwa na kupewa daraja.




CHANZO CHA HABARI; FILAMU CENTRAL
Asante!

Posted by Bongo Film Data Base on 11:47 PM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0

0 comments for SERIKALI YATOA NEMBO YA KUZITAMBUA KAZI ZA WASANI SASA...

Post a Comment

LETS HOOK UP

.

.
.
slide

SIRI YA MTUNGI PHOTO CAPTION


Recently Commented

ALBUM YA BONGOFILM

SIMULIZI ZILIZOBAMBA KWENYE KURASA ZA KIJAMII

TAKE ONE -HBABA NA FLORA INTERVIEW

2009 Bongofilmdatabase. All Rights Reserved. - Designed by Oscar kwa ushirikiano wa SimplexDesign