KOZI FUPI TOKA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM YA KUANDIKA MISWADA YA FILAMU HUTOLEWA MWEZI HUU

 Idara ya sanaa na sanaa za maonesho chuo kikuu cha dar es salaam kwa kushirikiana na FPA Alumanae  waanda Warsha ya Uandishi wa Miswada ya Filamu (Screenplay) itakayo anzaa tarehe 13 mpaka 15 mwezi huu wa  Februari 2012

Muda ni  Saa tatu (3) asubuhi hadi majira ya saa saba (7) mchana na mahali mafunzo yatakapotolewa ni pale Idara ya Sanaa na Sanaa za Maonesho, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. mafunzo yamewalenga zaidi Waandishi wa miswada ya filamu, watengenezaji, waongozaji na hata  wapenzi wa filamu pia wanakaribishwa.

Lugha itakayotumika kuendeshea mafunzo haya ni  Kiswahili ila Kiingereza kitatumika pale inapobidi

Ada ya mafunzo haya ni shilingi elfu hamsini za kitanzania tu:(50,000) Pamoja na mengine mbali na elimu juu ya uaandishi mshiriki atapata Cheti cha Ushiriki, makala na machapisho mbalimbali juu ya uandishi wa miswada ya filamu, viburudisho...

Vitu vya ziada ambavyo tutapendezwa kukuona nacho kwenye mafunzo ni kipajaisho (laptop) kama unacho

Waendeshaji: John Mwakilama, Vicensia Shule,...

Kwa maelezo zaidi wasiliana na: John Mwakilma 0714 13 22 49, mwakilamajohn@yahoo.com

Posted by Bongo Film Data Base on 6:08 PM. Filed under , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0

0 comments for KOZI FUPI TOKA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM YA KUANDIKA MISWADA YA FILAMU HUTOLEWA MWEZI HUU

Post a Comment

LETS HOOK UP

.

.
.
slide

SIRI YA MTUNGI PHOTO CAPTION


Recently Commented

ALBUM YA BONGOFILM

SIMULIZI ZILIZOBAMBA KWENYE KURASA ZA KIJAMII

TAKE ONE -HBABA NA FLORA INTERVIEW

2009 Bongofilmdatabase. All Rights Reserved. - Designed by Oscar kwa ushirikiano wa SimplexDesign