TINO SASA AINGIA HATIANI.
habari, mpya, slide 12:20 AM
“Filamu ya Hatia ni moja kati ya filamu kali ambazo msanii huyu ameigiza, na Hatia ina utofauti sana katika filamu ambazo ninazifanya, kwanza tumeirekodi nje ya Jiji la Dar es salaam, katika filamu hiyo unapata mazingira tofauti ambayo tumezoea kuyaona kila siku, pia imeshirikisha wasanii wakali wenye uwezo,”anasema Tico.
Kisa cha filamu hiyo kinamhusu kijana INNOCENT “Tino” ambaye anakutana na vikwazo vingi katika maisha yake, kutokana na hali halisi ya maisha ya chini aliyonayo anaamua kupiga moyo konde na kuamua kukabiliana na hali iliyopo, lakini kwa bahati mbaya anaingia hatiani kwa kosa la mauaji na kukutwa na silaha kinyume cha sheria, ni hadithi yenye uzuni burudani na mafunzo.
Filamu ya Hatia inawakutanisha wasanii wakali katika tasnia ya filamu Tanzania kama vile Simon Mwapagata ‘Capturado’, Abdalah Mkumbila ‘Muhogo Mchungu’, Hisani Muya ‘Tino’, Kemmy, na Bi. Aisha, filamu hiyo imeongozwa na muongozaji mahiri wa filamu Tanzania Kulwa Kikumba ‘Dude,
CHANZO; FILAMUCENTRAL
Asante!