DHUMUNI YA SAFARI YA WEMA SEPETU HUKO DUBAI NI HII HAPA
habari, mpya, slide, udaku 2:23 PM
Habari zilizotufikia juu ya dawati letu ndani ya chumba cha habari siku kama tatu ni kuhusiana na dada wema kupanda pipa mpaka Dubai na kurejea hapa nchini na vifaa vya kutayarishia filamu ambavyo kiuhakika vitakuwa chini ya himaya yake ambayo itaanza kutayarisha filamu zake.
Hatua hii ni nzuri sana ila je! jopo la utayarishajii hizo kazi zake wana taaluma na ujuzi na kile wanachokwenda kutayarisjha? au ndiyo zile , haloo!...upo wapi mshikaji wangu? nina kimeo kimojakama vipi cha kama scene kumi njoo unipigie fasta fasta , kuna hela ya mafuta mshikaji wangu ... naye mpigiwaji anakata simu mara baada ya kusema ''haina noma naja''
Wadau wa tasnia hii ya filamu hapa nchini chonde chonde tuheshimuni thamani ya sanaa na tuifanye katika viwango vilivyo bora kwa kuwashirikisha watu wenye taaluma zao za mambo haya kwani walikwenda shule na kuja kulitumikia taifa hili kwa maarifa hayo na kupitia nyinyi mliyo bahatika kupata nafasi kwenye jamii hii na kukubalika hatimaye uwezo wa kumliki vifaa hivi. basi tuwatafute watu hawa na tuwatumie vyema. kama sivyo sanaa hii hsitskwenda mahala popote pale zaidi ya kuona maigizo yale yale ya kila siku uliyoyazoea ya baby i love you so much,baby nimefukuzwa kazi na kodi ya pango wanaloishi wanadaiwa...
Bongo Film Data Base inawapapongezi wale wote wenye maamuzi ya kuthubutu kama huyu dada wema na twakusii usife moyo usipofanikiwa kuzalisha filamu kama ulivyotengemea kwani bado vifaa zitakuwa kwenye himaya yako na kuweza kuvifanyia mambo mengine kama kuvikodisha kwa wadau wengine wenye ufahamu wakuvitumia ila hwana uwezo wa kumiliki vifaa kama hivyo...
Tweet
Sio kwamba Tanzania hautuna vifaa, bali hatuna elimu na ubunifu, kingine hatuna wivu wa maendeleo, jumlisha vyote sawasawa ni UJINGA!