MJUE VILIVYO BOND BIN SINNAN LEO



Bond Bin sinnan
[Director,producer,actor,Story writer and Presenter]

Kijana huyu alipatiwa jina la  Abdallah Suleiman Bin Sinnan  na wazazi wake mara baada kuzaliwa munamo mwaka 1983 huko kanda ya ziwa kwenye mkoa mmoja maarufa sana hapa Tanzania kwa kupatika samaki baridi mkoa uitwao mwanza pale hospitari ya bugando .
Abdallah alianza kujihusisha na mambo ya sanaa mwaka 1999 mpaka sasa anatimiza kama kumi na moja katika tasnia hii ingawa hukuanzia moja kwa moja kwenye  tasnia ya maigizo, alianza na upande wa uimbaji pale awali. Hakufanikiwa kupata elimu za sanaa katika shule zitoazo masomo ya husianayo na sanaa yake kwa hapa nchini bali alifanikiwa kuitafuta elimu hii kwa njia ya mtandao kwa lengo la kujiweka sawa ukiachilia mbali kipaji chake binafsi.

Abdallah hutumia muda wake waziada kujifunza vitu vya ziada kuza na kutizama ni changamoto zipi wadau wakubwa katika tasnia zinawakabili katika ulimwengu huu wa sinema kwa kutizama filamu zao wakiwemo watayarishaji na waongozaji wa kazi za ndani na nje ya Tanzania.  

Vitu ningine anavyovipenda ni kuimba na kutangaza pia kitu ambavyo anavihusudu kwa sana,kipindi kile cha nyuma alikutana na wakati mgumu sana kuingia kwenye hii tasnia kutokana na kuwepo na uelewa mdogo wa watu na mambo haya ya maigizo tena ukizingatia ilikuwa ni huko mkoani hivyo alikabiliana na changamoto hiyo na ilikuwa ikimweka kwenye wakati mgumu sana kwa kila aliyemweleza ya kuwa yeye ana uwezo wakuigiza alionekana kama anaongopa.  

Hali hiyo ilikuja kubadirika kabisa mara tu alipopata nafasi ya kutokeza na kuonekana kwenye luninga na kufanya vizuri kutokana na yeye kuwa na uzoefu na haya mambo ya upigaji tangu akiwa mdogo sana hivyo ule muwashasha haukumsumbua sana na hata kujiona mbele ya wenzake ingawa yeye anasema umaarufu husumbua sana kwa mtu aliyeupata bila kujipanga na hatimaye wana kuwa juu kasha shuka mara moja tofauti na  yeye kwani humwomba sana Mungu na amejaliwa kupata hata washauri wazuri kutoka kwa watu wanaomzunguka akiwemo mchumba wake. 

Kutoka na tasnia hii hapa nchini Tanzania kuwa ile ya kaka,rafiki katoka na mimi atanisaidia name kwenye upande huu ya tasnia ni wengi sana ambao amefanikiwa kushirikiana nao katika kazi tofauti tofauti nao kurudi kumshukuru kwa msaada na mchango aliouchangia kama yeye na hata wengine kuthubutu kumtizama kama mfano wao[role model] na kwa upande wake watu ambao huwatizama ni Jacob Steven [Jb] kwa hapa nyumbani, Amir Khan na Mel Gibson toka huko marekani kutokana na kujituma kwao katika kazi.



Wanasanii wengi hapa dunia hucheza filamu kadhaa na mwisho wa siku hupata utambulisho wao rasmi wa uhusika ambao akipewa mwongozo hufanya vizuri sana mfano Jack Baure ameonekana kufanya vizuri sana kwenye filamu za kipelelezi na za kivita kuliko za aina nyingine na hata kutochaguliwa kabisa kufanya filamu tofauti na za namna hiyo, ila kwa abdallah hii ipo tofauti sana kwa upande wake wa kujitafutia utambulisho wake wa uhusika na kuamua kufanya kila aina ya uhusika atakaye letewa kucheza atauvaa bila shida yeyeto ile igawa anasisitiza kutocheza uhusika wa ushoga hata siku moja..

Pamoja na kuwa anajiamini kiasi chote hicho cha kuweza kucheza nafasi tofauti tofauti kwenye filamu aliwahi kushidwa kufikia kiwango kilichohitajika na mwongozaji wa tamthilia ya Unfaithfull ambapo aliongozwa acheze kama muhudumu wa bar.siku hiyo hataweza kuisahau maishani mwake kwani alishindwa mbele ya waongizaji wakubwa toka nje ya nchii hii ya Tanzania ijapokuwa alijifunza mengi sana kutokana kushindwa kwake huko.

Abdallah amefanya kazi kadhaa mpaka sasa ila kazi ambayo alimelipwa vizuri naye kuona anatambuliwa vyema kwa mchango wake kwenye kuifaniksha kazi hiyo ni filamu ya Lost Souls iliyotoka wiki kadhaa zilizopita.
   Na mtizamo wa tasnia hii hapa Tanzania kwa upande wa abdallah alikuwa na haya ya kusema; Imepanda sana kuanzia Kiubora mpaka mapato hilo liko wazi ingawa bado kila kitu hakilingani na hadhi yake, ila baadhi ya  wasanii hawalipwi  vyema kama filamu zao  zinavyowafaidisha wasambazaji hivyo bado kuna tatizo hilo ambalo ni kubwa na lisipoangaliwa tutarudi tulikotoka’’. Na kwa washaiki wangu wote, jamani mie kijana wenu sina cha kusema sana ila nawaomba muendelee kunisapot na kuniunga mkono pia msiache kunikosoa ninapokosea na kunishauri ili niendelee kusonga mbele, 
Mungu awabariki sana . Mwabeja sanaa ' maana yake asanteni sanaan kwa lugha ya mama yangu kisukuma hahahaa..

TUMA BIOGRAPH YAKO LEO KUPITIA MAIL YETU NAWE TUKUANDALIE KITU CHA

 NAMNA HII

Mail; bongofilm@hotmail.com

 ...KARIBU SANA.

SHUKRANI NYINGI KWA ABDALLAH a.k.a Bond Bin Sinnan

Posted by bongofilmdatabase on 12:47 PM. Filed under , , , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0

0 comments for MJUE VILIVYO BOND BIN SINNAN LEO

Post a Comment

LETS HOOK UP

.

.
.
slide

SIRI YA MTUNGI PHOTO CAPTION


Recently Commented

ALBUM YA BONGOFILM

SIMULIZI ZILIZOBAMBA KWENYE KURASA ZA KIJAMII

TAKE ONE -HBABA NA FLORA INTERVIEW

2009 Bongofilmdatabase. All Rights Reserved. - Designed by Oscar kwa ushirikiano wa SimplexDesign