ELIMU KWA WASANII WA FILAMU NCHINI‏


Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) na asasi ya Gaba Arts mapema wiki hii wameendesha semina fupi kwa Wasanii wa filamu ili kuwajengea weledi katika eneo la uandishi bora wa miswada ya sinema (script writing).

Semina hiyo iliyoendeshwa kupitia programu ya Jukwaa la Sanaa kwenye Ukumbi wa BASATA ilijikita katika maeneo ya namna ya kuendeleza wazo hadi sinema ya kusisimua, namna ya kufikia hisia za watazamaji,ujenzi mzuri wa matukio,kutengeneza wahusika na mfumo wa hadithi, Mwanzo, kati na hitimisho.

Akitoa mada kwenye programu hiyo maalum, Mkurugenzi wa asasi ya Gaba Arts James Gayo alisema kuwa, muda umefika sasa kwa wasanii wa filamu kusaka maarifa ili kutengeneza sinema zenye visa vipya, zenye weledi na zisizosukumwa na matakwa au maelekezo ya wasambazaji.

“Wenzetu kutoka nje wanatamani sana kupata vitu kutoka Afrika vyenye kuzungumza uhalisia wa maisha ya kwetu, wanataka kuona vitu vipya hivyo, katika uandishi wa muswada wa sinema suala la uhalisia na visa vyenye utofauti ni la msingi sana” alisisitiza Gayo.
Alizidi kueleza kuwa watazamaji wa sinema (filamu) huwa wana kawaida ya kuchoka pale wanapolishwa visa vya aina moja muda wote na akaonya kuwa kama wasanii hawatajikita katika kubuni visa vipya na vyenye kugusa uhalisia wa maisha yao wadau watasusia kununua.
“Ikiwa tutaendelea kutengeneza filamu zisizo na weledi, zenye visa vilevile na zenye kusukumwa na wasambazaji au haja ya kuchuma fedha za haraka tu watu watatuchoka na baadaye soko litakufa” alionya Gayo.

Gayo ambaye amepitia mafunzo ya utengenezaji filamu katika mataifa mbalimbali ikiwemo Marekani alitaja sifa za muswada (script) bora kuwa ni pamoja na kubeba wazo linalozalika kwenye jamii, visa vyenye uhalisia na vipya, utengenezaji mzuri wa wahusika na sifa zingine nyingi.

Kwa upande wake msanii wa mashairi Mrisho Mpoto ambaye alikuwa miongoni mwa waliohudhuria semina hiyo alisema kuwa, wasanii wa filamu wanahitaji kusaidiwa kwani kwa sasa soko la filamu limekuwa la kitumwa na lenye kuburuzwa na matakwa ya wasambazaji bila weledi.

Akihitimisha programu hiyo, Katibu Mtendaji wa BASATA Ghonche Materego alishauri wasanii wa filamu kujipanga kushirikiana na wasomi wenye weledi katika maeneo yao ili kuzalisha kazi zenye weledi la ubora.
E
“Tuna wataalam wengi katika Sanaa, wamebanana na mambo mengi lakini ni vema wasanii tukawatumia na kushirikiana nao katika kuboresha kazi zetu” alisisitiza Materego.
Captions
1.   Mkurugenzi wa asasi ya Gaba Arts James Gayo akisisitiza jambo wakati akitoa mafunzo kwa wasanii wa filamu juu ya Stadi za Uandishi wa Miswada ya Sinema (Script) kwenye Jukwaa la Sanaa linalofanyika kila wiki makao ya Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA).
2.   Bw. Gayo akifafanua hatua katika uandishi wa muswada bora wa filamu (script)
3.   Katibu Mtendaji wa BASATA Ghonche Materego akitoa ufafanuzi kuhusu uandishi wa Miswada bora ya simema (Scripts) kwenye Jukwaa la Sanaa wiki hii.
4.   Mtunzi na mwongozaji wa Sinema wa Kundi la maigizo la Jakaya Theatre linalorusha michezo yake kila Jumamosi kupitia ITV, Chedieli G. Senzighe akichangia kwenye mjadala.
5.   Msanii wa Sanaa ya ushairi Mrisho Mpoto naye alitoa mchango wake na kuuliza maswali kadhaa juu ya uandishi bora wa miswada katika sinema.
6.   Sehemu ya Wasanii waliohudhuria elimu hiyo wakifuatilia moja ya filamu zilizotengenezwa kutokana na muswada (script) makini.
7.   Wadau waliohudhuria programu hiyo wakifuatilia kwa makini. 

Na. mwandishi wetu

Posted by bongofilmdatabase on 9:14 AM. Filed under , , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0

0 comments for ELIMU KWA WASANII WA FILAMU NCHINI‏

Post a Comment

LETS HOOK UP

.

.
.
slide

SIRI YA MTUNGI PHOTO CAPTION


Recently Commented

ALBUM YA BONGOFILM

SIMULIZI ZILIZOBAMBA KWENYE KURASA ZA KIJAMII

TAKE ONE -HBABA NA FLORA INTERVIEW

2009 Bongofilmdatabase. All Rights Reserved. - Designed by Oscar kwa ushirikiano wa SimplexDesign