BIFU NA UTATA MWINGINE TENA HUU HAPA WATENGENEZWA NA MAGAZETI


Kwa kitambo kirefu  sasa jopo la Bongo Film Data Base inafuatilia kwa ukaribu sana hadithi  zisimuliwazo kwenye vyombo vya habari hapa nchini nakugundua mengi sana likiwemo la habari hizo kutokuwa na ukweli wa aina yoyote na kibaya zaidi zina kuwa hazina uthibisho wa kutosha toka kwa wahusika zaidi ya kuwashinikiza wanayo yazungumza kwenye hadithi hizo na  zaidi kuliko ni ubumbaji wa matukio hayo kwa kuowanisha picha tu. 

Mfano wa hadithi ya Jackline wolper kufananishwa na Amber Rose kutokana na picha alizopiga juzi kati ambazo alikuwa katika pozi na mwonekano wa tofauti na hapo zamani ulioshabiana na mwana mitindo anayetamba sana huko  marekani, mwite Amber. 


Hadithi hiyo iliambatanishwa na kuwepo kwa picha za utupu za Jackline wolper ila mpaka sasa picha hizo hazipo hewani wala gazeti lolote lile.... 




PICHA HIZI NDIZO ZILIFANANISHWA 






HADITHI NYINGINE HII HAPA  IPO JIKONI SASA ITIZAME EWE MDAU WETU
NA UKARASA WA KWANZA WA TAMTHILIA  NDIYO UMEANZIA HAPA SASA  ;..(twanukuu kama ifuatavyo)
KISHINDO cha Jokate Mwegelo ni kizito, kimeingia ndani ya uhusiano wa brazameni, Naseeb Abdul ‘Diamond’ na Wema Sepetu kisha kuwafanya wawili hao kila mmoja kushika hamsini zake.
Wema, amefunga virago, ameondoka nyumbani kwa Diamond, Sinza Madukani, Dar es Salaam kwa mtindo wa “wanakwenu kwa heri, nimechoka masimango, narudi nyumbani kwetu leo.”
Madai ‘yanahiti pointi’ kuwa Diamond na Jokate wapo kwenye penzi jipya lenye nguvu, Wema ameligundua hilo, ameona ni maji marefu, kwa hiyo amejiweka pembeni kuepuka msongamano.

Inazidi kudaiwa kwamba Wema alijaribu kumfanya Diamond atulie lakini ikashindikana, ilipodhihirika Jokate ameshika mpini, alianza kupata mateso ya moyo na hisia kwa jinsi alivyofanywa ‘spea tairi’.

Madai ‘yanahiti’ pia kwamba Wema alithibitisha kuwa Diamond na Jokate wanamchezea ‘ukuti ukuti’ baada ya kuwafumania wakiwa ‘vere klozi’ kimahaba kwenye Hoteli ya Picolo, Masaki, Dar es Salaam.

Hata hivyo, inadaiwa kuwa Wema alipowakuta Diamond na Jokate, hakuangusha varangati kama mmiliki, badala yake alinywea utadhani yeye ndiye mwizi kisha akawaambia: “Samahanini sana kwa kuwaingilia kwenye starehe zenu.”

TOKA KWENYE KIVULI CHA HISTORIA 
VITA YA TANGU ENZI
Wema na Jokate, walipambana kwenye vita ya kuwania Taji la Miss Tanzania mwaka 2006 lakini safari hii wanapambana kwa ajili ya penzi la mwanaume.

Mwaka 2006, Wema aliibuka kidedea kwa kuchukua taji, wakati Jokate alishika nafasi ya pili, safari hii inaonekana kibao kimegeuka, kwani Miss Tanzania huyo bila kulazimishwa, mwenyewe kainua mikono na kutimka.

NENO LA WEMA
Wema akizungumza na paparazi wetu baada ya kurejea nyumbani kwao, Sinza, Mori, Dar es Salaam, alisema kuwa ameondoka kwa Diamond baada ya kujiridhisha kwa ushahidi wa kina kwamba anatoka na Jokate.

Mrembo huyo alisema, anaumia kwa sababu aliamua kutulia na Diamond kwa mapenzi yote na uaminifu, kumbe mwenzake hakuwa na utulivu.

“Unajua watu wengi wanajua mimi situlii  na mwanaume mmoja kitu ambacho nakipinga kabisa, kwa maana kuna wakati navumilia ninayofanyiwa  na wanaume lakini inashindikana,” alisema Wema.

Staa huyo aliendelea kusema kuwa baada ya kujua uhusiano unaoendelea  kati ya Diamond na Jokate, aliamua kujifanya mjinga ili mchumba wake huyo ajirekebishe lakini bado akawa anasikia habari hizo.

“Nimeona bora nirudi nyumbani kwetu nikapumzike kwanza, kwa maana nyumbani kwetu sijafukuzwa wala hakuna shida yoyote,” alisema Wema.

JOKATE NAYE PICHA KUTOKA UKURASA WA CHOKA 
Jokate alipozungumza na ripota wetu, alisema kuwa hana bifu na Wema kwa sababu hajawahi kumfanyia ubaya wowote.
“Sijatembea na Diamond, nilikuwa karibu naye kikazi. Wimbo mpya wa Diamond unaoitwa Mawazo, video yake na mimi nimecheza.

“Ni kweli kuna maeneo kadhaa nilikuwa naambatana na Diamond lakini siyo kimapenzi. Nilikuwa naye kikazi, siyo kimapenzi hata kidogo,” alisema Jokate.



KIUKWELI TASNIA HII YA FILAMU ILIWABOA WENGI SANA KWA KIPINDI CHA NYUMA KUTOKANA NGUVU NYINGI KUTUMIKA NA KIPATO KUTOONEKANA ILA KWA  SASA WANAITAMANI  SANA NA HATA WENGINE KUENDESHA MAISHA YAO VIZURI ZAIDI YA HAPO AWALI...... 
 UKITIZAMA PICHA HIZI MBILI AMBAZO NI VIPANDE VYA VIDEO MPYA YA DIAMOND NDIZO ZINATUMIKA KUTENGENEZA BIFU NA CHOKO CHOKO KATI YA HAWA WATU WENYE MAISHA YAO POA KABISA KWA SASA. WATANZANIA TUAMKE JAMANI 
KWA WALE WANAPENDA KUSHIRIKI KWENYE HII TAMTHILIA  TUAACHIE KOMENT ZAKO HAPO KWENYE KISANDUKU CHETU CHA MAONI....


CHANZO HIKI; GLOBAL PUBLISHER.



Posted by Bongo Film Data Base on 12:34 PM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0

2 comments for BIFU NA UTATA MWINGINE TENA HUU HAPA WATENGENEZWA NA MAGAZETI

  1. WEE ACHA TAMAA UMEONA WEMA ANAFAID SANA KUWA NA MSIMAMO KAMA MWANAMKE USIPENDE KUVURUGA MAPENZI YA WATU MUNGU HAPENDI HIVYO DO YOU UNDERSTAND

  2. hivi hawa wasanii wa Bongo hawawezi kuokoka na kumkabithi Bwana yesu awe mokozi wa maisha yao?hawaoni kwamba mwenendo wa maisha yao utabadirika na bado wataendelea kung'aa zaidi katika kazi zao.....
    Jamani Watanzania haijarishi kama wewe ni msanii ama la ukweli unabaki palepale kwamba wewe ni mtanzania hebu tuwe na hofu ya Mungu japo kidogo halafu tuone jinsi Mungu atakavo tuinua.
    Mrs. Mwakyusa

Post a Comment

LETS HOOK UP

.

.
.
slide

SIRI YA MTUNGI PHOTO CAPTION


Recently Commented

ALBUM YA BONGOFILM

SIMULIZI ZILIZOBAMBA KWENYE KURASA ZA KIJAMII

TAKE ONE -HBABA NA FLORA INTERVIEW

2009 Bongofilmdatabase. All Rights Reserved. - Designed by Oscar kwa ushirikiano wa SimplexDesign