FILAMU CENTRAL; BILA YA RAY HAKUNA BONGO MOVIE

NI Wajibu wetu kuwapongeza wale wote ambao wamekuwa chachu ya tasnia ya filamu hapa Bongo, pamoja na mapungufu yaliyopo kuna watu ambao wanastahili pongezi za kipekee katika kuleta chachu na kujenga thamani ya tasnia hii ya filamu, bila woga basi pongezi hizi zimwendee moja kwa moja mpiganaji nambari moja Bongo Vincent Kigosi ‘Ray the Greatest’


Ray amekuwa ni moja kati ya chachu na mafanikio ya tasnia ya filamu Bongo, pengine kuna watu ambao wanaamini kuwa tasnia hii ya filamu ameishikilia kwa asilimia kubwa katika kuleta maendeleo, pamoja na kutengeneza filamu na kupigania maslahi katika filamu lakini pia yeye ndiye amekuwa mbunifu na mleta mabadiliko Bongo.


Kwa hili ukubali ukatae lakini ukweli unabaki pale pale,ndio maana siku moja nilikuwa nikiongea na mtu mmoja nikamwambia Ray ni dira ya tasnia ya filamu Bongo akakata lakini kuna siku yeye mwenyewe alikuja na kukiri kuwa kweli maneno yako uliyosema.
Kama leo hii mpiganaji huyu akisema kuwa tasnia hii ibadilike na kwenda katika hatua nyingine hakuna ubishi lazima tutafika tunakotaka kwenda, ni wazi kuwa jamaa anajua anachofanya naweza kumkataa Ray kwa sababu zangu ambazo si za msingi lakini linapokuja suala la chachu ya mabadiliko katika tasnia hii mtu huyu ni muhimu.

Awali nikiongea naye alinieleza kuwa hapo mwanzo alikuwa akitumia vifaa kwa kukodi lakini aligundua kuwa ni gharama na aliamua kusafiri kwenda nje kwa ajili ya kununua vifaa vyake kwa ajili ya Production, na baada ya kurudi Swahiba yake alikwenda naye Marekani kwa ajili ya kununua baadhi ya vifaa kwa ajili ya Production.
Mara nyingi Ray amekuwa akianza kufanya jambo na wengine wanafuatia, anastahili kupongezwa yeye ndiye aliyekuwa wa kwanza kabisa kuamini kuwa wasanii wanaweza kuwa watayarishaji na alifanya hivyo japo wapo waliokuwa wakisema hataweza na kurudi kwa Mtitu Game, lakini jamaa alisimama imara.
Msanii huyu baada ya kutoka na filamu ya Johari na kufanya vizuri kupita maelezo alianza harakati zake katika kupigania maslahi yake na hatimaye alitengeneza filamu ya Fake Pastor lakini hakubweteka hapo kwani alikuwa hajafika na aliamua kama yeye kutoa filamu ya Shakira.
Baada ya muda aliingia mkataba na Mtitu kwa filamu kadhaa na alirudi na kuendelea na kuamua kufungua kampuni yake kwa ushirikiano na msanii mwenzake Blandina Chagula hapo ilizaliwa kampuni ya RJ Company ambayo inasumbua Bongo na nchi jirani katika masuala ya filamu.

Najaribu kuongelea sehemu mbalimbali ambazo Ray alipitia ili kukupa uhalali wa kumtangaza kama mwanaharakati na shujaa katika kuleta mabadiliko katika tasnia ya filamu Bongo jamaa ni mpiganaji wa kweli lakini pia mwenye huruma na wasanii wengine kwani sehemu aliyopo ukaribisha na wengine.
Baada ya kampuni ikumbukwe kuwa alitumia nafasi ya ubunifu kuweza kubandika stika katika gari lake la Production na wengine walifuatia, kufanya hivyo kwa kila mtayarishaji anatamani kuwa kama Ray kwa kila kitu lakini kwa upande mwingine inakuwa ngumu.
Hata kuna baadhi ya wasanii wamekuwa wakitumia nguvu ya msanii huyu kujihalalishia mambo Fulani Fulani, kwetu sisi Ray ni Shujaa katika tasnia ya filamu jamaa ana mambo mengi ambayo jamii inatakiwa kuiga kutoka kwake ni mjasiriamali, mpiganaji asiyechoka.
Lakini pia ni mtu mwenye msimamo kwa kile anachoamini jambo ambalo limekuwa ni chachu ya maendeleo yake katika utendaji wa kazi zake za filamu na maisha kwa ujumla.
Mwaka huu tunaanza na uchambuzi huu wa kuwatambua wapiganaji wanaoleta changamoto katika filamu Bongo, kwani yeye ndio alikuwa mtu wa kwanza hata kugundua kuwa ili uuze kazi yako inaanzia kwenye muonekano kwa kulitambua hilo alimgundua bingwa wa makava Bongo Raqey na kumpatia kazi hiyo.
Hadi sasa ili msanii mkubwa filamu yake iweze kuingia sokoni kwa uhakika lazima kava lake litengenezwa I View Media, lakini Ray amekuwa akigundua vipaji vipya kila leo na kuvipa uhusika jambo ambalo limezidi kuongeza wasanii katika tasnia ya filamu, mambo ni mengi kutoka kwa mtu huyu.

the second wife
Lakini ndiye msanii pekee ambaye hata ukimkosoa anaweza kutumia busara kuongea na wewe na kujadili jambo husika, kulingana na mfumo uliopo unawabana sana wasanii kujitanua zaidi kimaslahi jambo ambalo linapunguza utendaji wao, bila uoga wala chuki tunasema kuwa Bila Ray Hakuna Bongo movie kwa maana ya filamu.



CHANZO; FILAMU CENTRAL
Asante!

Posted by Bongo Film Data Base on 12:42 PM. Filed under , , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0

0 comments for FILAMU CENTRAL; BILA YA RAY HAKUNA BONGO MOVIE

Post a Comment

LETS HOOK UP

.

.
.
slide

SIRI YA MTUNGI PHOTO CAPTION


Recently Commented

ALBUM YA BONGOFILM

SIMULIZI ZILIZOBAMBA KWENYE KURASA ZA KIJAMII

TAKE ONE -HBABA NA FLORA INTERVIEW

2009 Bongofilmdatabase. All Rights Reserved. - Designed by Oscar kwa ushirikiano wa SimplexDesign