RIDHIWANI; SUBTITLE BADO NI UTATA KATIKA FILAMU ZA KITANZANIA
habari, mpya, slide 12:34 PM
RIDHIWANI Kikwete mtoto wa Mh. Rais Dr. Jakaya Mrisho Kikwete wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ijumaa alikuwa mgeni rasmi katika sherehe za kutimiza mwaka mmoja toka kundi la Bongo movie Club lianzishwe, sherehe hizo ambazo zilifana sana zilifanyika katika ukumbi wa Business Park Victoria Ridhawani alisema kuwa filamu nyingi zimekosa ubunifu na (Subtitle) tafsiri mbovu.
“Nawapongeza kwa umoja wenu lakini nina jambo moja lazima niliseme kwenu filamu zenu nyingi zimekosa ubunifu, unaloliona katika filamu iliyopita unaliona katika filamu mpya hali inayoonyesha hakuna ubunifu, sisi tunaangalia filamu hizi kupitia DSTV ukiangalia zile subtitle ni matizo kweli kweli maana sisi pamoja na kusoma kidogo tunaona mapungufu makubwa sana,”anasema Ridhiwan.
Mdau huyo mkubwa wa vijana amewashauri watengenezaji wa filamu kufika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kuwaona Maprofesa na wataalamu wa Lugha kwa ajili ya kuwatafsiria kiingereza katika lugha bora na yenye kuleta maana na si kama ilivyo sasa ambapo wanaharibu lugha za watu.
“Wafuateni wataalam pale chuo kikuu wapo watawasaidia waambieni tusaidieni kama watasema wanataka milioni wapeni hata laki tano kwa kuwaomba ili kuijenga tasnia hiyo ya filamu, pia kuweni wabunifu zaidi tuone kitu tofauti na si kitu kile kile,”anasema Ridhiwan.
.
Sherehe hiyo ilifana sana kwani wasanii hawa nyota pamoja na kuwa mahiri katika uigizaji lakini pia kumbe ni mahiri katika fani ya muziki baada ya kuimba nyimbo na kusakata rumba kwa kiwango cha juu, na kivutio zaidi alikuwa ni Steve Nyerere, Chiki Mchoma rapa nambari moja Bongo movie huku Richie, Mainda, Kupa na JB wakibuka kwa kumwaga viuno vya kufa mtu ilipendeza.
on Mar. 19th, 2012 by
“Nawapongeza kwa umoja wenu lakini nina jambo moja lazima niliseme kwenu filamu zenu nyingi zimekosa ubunifu, unaloliona katika filamu iliyopita unaliona katika filamu mpya hali inayoonyesha hakuna ubunifu, sisi tunaangalia filamu hizi kupitia DSTV ukiangalia zile subtitle ni matizo kweli kweli maana sisi pamoja na kusoma kidogo tunaona mapungufu makubwa sana,”anasema Ridhiwan.
Mdau huyo mkubwa wa vijana amewashauri watengenezaji wa filamu kufika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kuwaona Maprofesa na wataalamu wa Lugha kwa ajili ya kuwatafsiria kiingereza katika lugha bora na yenye kuleta maana na si kama ilivyo sasa ambapo wanaharibu lugha za watu.
“Wafuateni wataalam pale chuo kikuu wapo watawasaidia waambieni tusaidieni kama watasema wanataka milioni wapeni hata laki tano kwa kuwaomba ili kuijenga tasnia hiyo ya filamu, pia kuweni wabunifu zaidi tuone kitu tofauti na si kitu kile kile,”anasema Ridhiwan.
.
Sherehe hiyo ilifana sana kwani wasanii hawa nyota pamoja na kuwa mahiri katika uigizaji lakini pia kumbe ni mahiri katika fani ya muziki baada ya kuimba nyimbo na kusakata rumba kwa kiwango cha juu, na kivutio zaidi alikuwa ni Steve Nyerere, Chiki Mchoma rapa nambari moja Bongo movie huku Richie, Mainda, Kupa na JB wakibuka kwa kumwaga viuno vya kufa mtu ilipendeza.
on Mar. 19th, 2012 by