RIDHIWANI; SUBTITLE BADO NI UTATA KATIKA FILAMU ZA KITANZANIA

Ridhiwan Kikwete
Ridhiwan Kikwete mdau wa filamu Swahiliwood.
Ridhiwani Kikwete, Jacob Stephen, Jacqueline Wolper, Subir Rupia, Steven MangereRIDHIWANI Kikwete mtoto wa Mh. Rais Dr. Jakaya Mrisho Kikwete wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ijumaa alikuwa mgeni rasmi katika sherehe za kutimiza mwaka mmoja toka kundi la Bongo movie Club lianzishwe, sherehe hizo ambazo zilifana sana zilifanyika katika ukumbi wa Business Park Victoria Ridhawani alisema kuwa filamu nyingi zimekosa ubunifu na (Subtitle) tafsiri mbovu.
Ridhiwani akilishwa keki na Jb huku wasanii wengine wakishuhudia.
“Nawapongeza kwa umoja wenu lakini nina jambo moja lazima niliseme kwenu filamu zenu nyingi zimekosa ubunifu, unaloliona katika filamu iliyopita unaliona katika filamu mpya hali inayoonyesha hakuna ubunifu, sisi tunaangalia filamu hizi kupitia DSTV ukiangalia zile subtitle ni matizo kweli kweli maana sisi pamoja na kusoma kidogo tunaona mapungufu makubwa sana,”anasema Ridhiwan.
Mdau huyo mkubwa wa vijana amewashauri watengenezaji wa filamu kufika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kuwaona Maprofesa na wataalamu wa Lugha kwa ajili ya kuwatafsiria kiingereza katika lugha bora na yenye kuleta maana na si kama ilivyo sasa ambapo wanaharibu lugha za watu.
Single Mtambalike, Sudi Ali, Ruth Suka
  
Riche akisakata Rumba kitaalam.

“Wafuateni wataalam pale chuo kikuu wapo watawasaidia waambieni tusaidieni kama watasema wanataka milioni wapeni hata laki tano kwa kuwaomba ili kuijenga tasnia hiyo ya filamu, pia kuweni wabunifu zaidi tuone kitu tofauti na si kitu kile kile,”anasema Ridhiwan.
.
Steven Mangere Wema Sepetu
Steve Nyerere akiwa na Wema mwanadada mwenye mikasa Swahiliwood.
Sherehe hiyo ilifana sana kwani wasanii hawa nyota pamoja na kuwa mahiri katika uigizaji lakini pia kumbe ni mahiri katika fani ya muziki baada ya kuimba nyimbo na kusakata rumba kwa kiwango cha juu, na kivutio zaidi alikuwa ni Steve Nyerere, Chiki Mchoma rapa nambari moja Bongo movie huku Richie, Mainda, Kupa na JB wakibuka kwa kumwaga viuno vya kufa mtu ilipendeza.



on Mar. 19th, 2012 by
shukrani...

Posted by bongofilmdatabase on 12:34 PM. Filed under , , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0

0 comments for RIDHIWANI; SUBTITLE BADO NI UTATA KATIKA FILAMU ZA KITANZANIA

Post a Comment

LETS HOOK UP

.

.
.
slide

SIRI YA MTUNGI PHOTO CAPTION


Recently Commented

ALBUM YA BONGOFILM

SIMULIZI ZILIZOBAMBA KWENYE KURASA ZA KIJAMII

TAKE ONE -HBABA NA FLORA INTERVIEW

2009 Bongofilmdatabase. All Rights Reserved. - Designed by Oscar kwa ushirikiano wa SimplexDesign