SWAHILI FILM AWARDS 2012 ZAJA KWA MARA NYINGINE TENA ,SASA KUUTAMBUA UBORA NA UMOJA WA KAZI ZA WASANII
habari, mpya, slide 1:11 PM
Ni miaka 50 sasa tangu Mtanzania asheherekee kupata Uhuru wa chi yake. Hii ni miaka ya kujivunia, iliyojaa historia kubwa ya maendeleo, mapambano na changamoto za kisiasa, kiuchumi, kijamii na kiteknohama katika maisha ya Mtanzania. Utamaduni ni Uti wa mgongo wa Mtanzania…. Hii ni kauli maarufu ya Rais wa kwanza wa Tanganyika Mwalimu Julius Kambarage Nyerere aliyoitoa siku chache tu baada ya kupata Uhuru.
Filamu ni moja ya njia za kuzitunza, kuzilinda na kuziendeleza tamaduni zetu. Na huu ni muda muafaka kwa kuwatunuku watayarishaji, waigizaji, waongozaji wa filamu, wahariri na wadau wote wa tasnia ya filamu Swahiliwood.
SWAHILI FILM AWARDS inatambua UBORA na UMOJA uliopo na unaohitajika ili kukuza tasnia hii ya filamu Tanzania, ni wakati wako wa kuwakilisha kazi yako ambayo ilitoka mwaka uliopita yaani mwaka 2011 kwa ajili ya kuingia katika tuzo kubwa na za kwanza kufanyika Swahiliwood kwa maelezo zaidi unaweza kutembelea mtandao wa www.swahiliawards.co.tz
Ni msimu wa furaha na kufuta machungu baada ya kutambuliwa kazi unayofanya huku tukizingatia kujenga UBORA na UMOJA wa kweli katika kujenga na kukuza tasnia hii ya filamu inayokua kwa kasi kubwa na kuleta tija tupo pamoja fomu zinapatikana kupitia mtandao lakini pia unaweza kuzipata sehemu kama Redio Uhuru Fm, kwa Wasambazaji wote na kwa maafisa Utamaduni nchini kote.
Tweet
Filamu ni moja ya njia za kuzitunza, kuzilinda na kuziendeleza tamaduni zetu. Na huu ni muda muafaka kwa kuwatunuku watayarishaji, waigizaji, waongozaji wa filamu, wahariri na wadau wote wa tasnia ya filamu Swahiliwood.
SWAHILI FILM AWARDS inatambua UBORA na UMOJA uliopo na unaohitajika ili kukuza tasnia hii ya filamu Tanzania, ni wakati wako wa kuwakilisha kazi yako ambayo ilitoka mwaka uliopita yaani mwaka 2011 kwa ajili ya kuingia katika tuzo kubwa na za kwanza kufanyika Swahiliwood kwa maelezo zaidi unaweza kutembelea mtandao wa www.swahiliawards.co.tz
Ni msimu wa furaha na kufuta machungu baada ya kutambuliwa kazi unayofanya huku tukizingatia kujenga UBORA na UMOJA wa kweli katika kujenga na kukuza tasnia hii ya filamu inayokua kwa kasi kubwa na kuleta tija tupo pamoja fomu zinapatikana kupitia mtandao lakini pia unaweza kuzipata sehemu kama Redio Uhuru Fm, kwa Wasambazaji wote na kwa maafisa Utamaduni nchini kote.
Tweet